1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ANC yaadhimisha miaka 112 ya kuasisiwa kwake Afrika Kusini

Bruce Amani
13 Januari 2024

Chama tawala nchini Afrika Kusini African National Congress - ANC kinasherehekea miaka 112 ya kuasisiwa kwake kabla ya kufanya uchaguzi wa kitaifa unaotarajiwa kuwa mkali zaidi tangu kilipoingia madarakani 1994

https://p.dw.com/p/4bCKA
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa
Ramaphosa anagombea muhula wa pili wakati kukiwa na ukosoaji mkubwa ndani ya ANCPicha: Denis Farrell/ASSOCIATED PRESS/picture alliance

Chama tawala nchini Afrika Kusini African National Congress - ANC kinasherehekea leo miaka 112 ya kuasisiwa kwake kabla ya kufanya uchaguzi wa kitaifa, unaotarajiwa kuwa mkali zaidi tangu kilipoingia madarakani katika mwaka wa 1994.

Soma pia: Ramaphosa mwenyekiti tena chama tawala ANC

Maelfu ya wanachama na wafuasi wanatarajiwa kukusanyika katika Uwanja wa Michezo wa Mbombela katika mkoa wa Mpumalanga ambako Rais Cyril Ramaphosa, ambaye pia ni mkuu wa chama wa ANC, atatoa hotuba yake ya mwaka na kutangaza mpango wa chama hicho kwa mwaka huu.

Soma pia: Chama cha ANC chagawanyika katika makundi yanayomuunga mkono na yanayompinga Ramaphosa

Ramaphosa anatafuta muhula wa pili katika uchaguzi wa mwaka huu baada ya kuingia madarakani katika mwaka wa 2019, akichukua usukani kutoka kwa Jacob Zuma. ANC imekuwa ikikabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kushindwa kutoa huduma za msingi kwa mamilioni ya raia weusi maskini walio wengi, wakati kukiwa na mazingira yanayozorota ya kiuchumi.