1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPanama

José Raúl Mulino achaguliwa rais mteule wa Panama

6 Mei 2024

Wapiga kura nchini Panama wamemchagua José Raúl Mulino kuwa rais kulingana na matokeo ya awali yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi.

https://p.dw.com/p/4fXPe
Uchaguzi Panama | Jose Raul Mulino
Mulino aliteuliwa kuwa mgombea mbadala wa mwanasiasa mrengo wa kulia Ricardo Martinelli, ambaye aliondolewa kwenye kinyang'anyiro hicho.Picha: DAVID TORO/EPA

Mulino, ambaye ni mshirika wa karibu wa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo aliyeandamwa na kashfa Ricardo Martinelli, ameshinda kwa asilimia 35 ya kura, baada ya asilimia 90 ya kura kuhesabiwa.

Rais huyo mteule anataka kukomesha uhamiaji haramu kupitia msitu wa Darien katika taifa hilo la Amerika ya Kati.

"Nitazungumza na kila mtu, nitamsaidia kila mtu, nitafanya mambo kuwa sawa. Sipendi makabiliano ya aina yoyote," amesema Mulino.

Mulino, ambaye ni waziri wa zamani wa mambo ya nje, usalama na sheria aliteuliwa kuwa mgombea mbadala wa mwanasiasa mrengo wa kulia Ricardo Martinelli, ambaye aliondolewa kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya kukutwa na hatia ya utakatishaji fedha na kuhukumiwa kifungo cha zaidi ya miaka 10 jela.