1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kuipatia Lebanon msaada wa dola bilioni moja

2 Mei 2024

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen yupo ziarani nchini Lebanon na amekutana kwa mazungumzo na waziri mkuu wa muda wa nchi hiyo Najib Mikati pamoja na viongozi wengine mjini Beirut.

https://p.dw.com/p/4fQHu
Beirut, Lebanon | EU Ursula von der Leyen,Rais, Rais wa Cyprus Nikos Christodoulides, Spika wa Lebanon Nabih Berri.
Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen,Rais wa Cyprus Nikos Christodoulides wakiwa na Spika wa Lebanon Nabih Berri mjini Beirut.Picha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Von der Leyen ambaye ameambatana na Rais wa kisiwa cha Cyprus Nikos Christodoulides ametangaza kuwa Umoja wa Ulaya utaipatia Lebanon msaada wa euro bilioni 1 ili kusaidia kukuza uchumi wa taifa hilo. 

Soma pia:EU kuliwekea vikwazo jeshi la Walinzi wa Mapinduzi wa Iran

Mkuu wa majeshi wa Lebanon, Joseph Aoun na waziri wa mambo ya kigeni Abdallah Bou Habib ni miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo.

Lebanon, yenye zaidi ya wakimbizi 800,000 wa Syria wanaoishi katika umasikini mkubwa, imekuwa ikikabiliwa na mgogorowa uchumi tangu mwaka 2019.